Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

WACHEZAJI WA MAN U WAMUOKOA KOCHA WAO VAN GAAL.



 
Klabu ya Manchester United usiku wa jana wameamka usingizini baada ya kuichapa klabu ya Derby mabao 3-1 katika raundi ya nne ya Kombe la FA.


Wayne Rooney alifunga kwa kombora alilolitoa akiwa hatua 20 kutoka golini mwa wapinzani wao na kuwaweka United mbele dakika ya 16 kabla ya George Thorne kupenya safu ya ulinzi ya vijana hao wa Van Gaal na kusawazisha dakika ya 37.

Kipindi cha pili Daley Blind aliwarejesha mbele baada ya kupokea krosi kutoka kwa Jesse Lingard dakika ya 65.

Juan Mata alikamilisha ushindi wao wa mabao hayo 3 katika dakika ya 83 ya mchezo na kuifanya itoke vifua mbele siku ya jana.

Derby, ambao hawajashinda mechi yoyote katika ligi yao mwaka 2016 wanashikilia nafasi ya tano katika ligi ya Championship.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget