Wizara ya Habari,Wasanii,Utamaduni na Michezo nchini imeanza kupokea
maoni na mawazo mbalimbali ya wadau nchini ikiwa na lengo la kuboresha zaidi sekta ya michezo nchini na kuifanya ifanye vizuri zaidi kwa washiriki wa sekta hiyo.
Akizungumza na kamati tendaji ya Baraza la michezoTaifa
BMT katibu wa Wizara hiyo ELISANTE OLE GABRIEL amesema lengo la kukutana na
kamati hiyo ni kujua changamoto amabazo zinaikabili kamati hiyo hasa kwa upande
wa vyama vya michezo nchini.
Naye Mwenyekiti wa kamati hiyo Dionez Malinzi
amesema kwa upande wa BMT kuna mambo mengi sana yanayo kwamisha sekta ya michezo
nchini na vyama vyake hasa kwa upande wa msajili wa vyama vya michezo nchini kusajili vyama vingi kiholela na
kulitaka suala hilo lifatiliwe kwa makini.
Post a Comment