Chama cha mchezo wa vishale unatarajiwa kufanya
uchaguzi wake wa viongozi wake waliomaliza muda wa kuongoza chama hicho
February 26 mwaka huu Mjini Dododoma.
Afisa habari wa Baraza la Michezo Taifa BMT Najaha Bakari
amesema maandalizi yote kuelekea katika uchaguzi huo yamekamilika na amewataka
wadau wenye sifa kuchukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali katika uchaguzi huo
na fomu zote zinazotolewa na BMT.
Kwa upande mwingine Najaha amevitaka vyama mbalimbali
vilivyo chini ya BMT kurejesha karenda ya mwaka ya vyama hivyo katika baraza hilo ili kujua
mipango ya vyama hivyo na malengo yao ya mwaka huu kama ilivyo kwa miaka
mingine wanavyofanya.
Post a Comment