Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

LIVERPOOL YAMTOLEA UDENDA TEIXEIRE AMBAYE NI KIUNGO MSHAMBULIAJI WA SHAKHTAR.



Alex Teixeira playing for Shakhtar Donetsk in the Champions League 

Klabu ya soka ya Liverpool ipo katika mazungumzo ya kutwaa kiungo wa klabu ya soka ya Shakhtar Donetsk's raia wa nchini Brazili Alex Teixeira katika kipindi hiki cha usajili barani ulaya.


Klabu ya Liverpoool ipo tayari kulipa kiasi cha £24.5m kwa ajili ya kutwaa mchezaji huyo mwenye miaka 26 katika viunga vya Anfield.

Hata hivyo Liverpool watakuwa na kibarua kizito baada ya mchezaji Teixeira huyo pia kutakiwa na klabu ya Chelsea kwa ada ya uamisho wa £39m.

Kocha wa klabu ya Liverpool Jurgen Klopp anaangaika kutafuta kiungo mshambuliaji hivi sasa baada ya wachezaji wake Danny Ings, Divock Origi Daniel Sturridge kuwa majeruhi.

Baada ya kumsajili Christian Benteke kwa £32.5m Liverpool wamefunga mabao 25 pekee kipindi katika michezo 22 ya ligi kuu soka nchini Uingereza katika kipindi hiki.

Teixeira hadi hivi sasa tayari ameshapachika mabao 22 katika michezo 15 ya ligi na mabao 4 katika michezo 10 ya ligi ya mabingwa barani Ulaya msimu huu.

Lakini kama Liverpool wakimsajili Teixeira atakuwa mchezaji wa 4 wa kibrazili kusajiuliwa na klabu hiyo baada ya kuwasajili wachezaji Lucas Leiva, Roberto Firmino na Philippe Coutinho katika klabu hiyo

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget