Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

KIBADENI ASEMA MGAMBO JKT WAJIANDAE KUPIGISHWA KWATA SIKU YA JUMAMOSI.



 

Klabu ya soka ya JKT Ruvu imefanya mazoezi yake hii leo kwaajili ya kujiandaa na mchezo wake wa ligi kuu soka Tanzania bara  dhidi ya Mgambo JKT mchezo utakaopigwa katika viunga vya uwanja wa karume jijini Dar es Salaaam.


Ligi kuu Soka inatarajiwa kutimua vumbi lake tena January 16 mwaka huu katika viwanja kadhaa baada ya kupumzika kwa muda kupisha kombe la mapinduzi lililofanyika visiwani Zanzibar.

Kocha mkuu wa klabu ya JKT Ruvu Abdalah King Kibadeni Mputa amesema lengo la mazoezi yao ya leo ni kujiweka sawa kwaajili ya mchezo wao huu huku akiwapongeza wachezaji wake kwa kujituma vizuri wanapokuwa mazoezini.
 
Kwa upande wake Nahodha wa klabu hiyo George Minja amesema hawana wasi wasi juu ya mchezo wao huo kutokana na mazoezi wanyoendelea kuyafanya huku wakipata mbinu nyingi za kuwakabili wapinzani wao kutoka kwa kocha wao.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget