
HATIMAYE mshambuliaji wa timu ya Taifa ya Tanzania
Taifa Stars, Mbwana Ally Samatta yupo njiani hivi sasa kuelekea nchini Ubelgiji
kujiunga na klabu yake mpya ya KRC Genk.
Samatta ambaye ni mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji
wa wanaokikipa nyumbani katika barani Afrika anatarajiwa anaonesha ishara nzuri
kutokana na umahiri wake wa kutandaza kabumbu.
Uhamisho wa Samatta siku chache zilizopita ulizua
utata baina yake na mmiliki wa klabu ya TP Mazembe, Moise Katumbi kabla ya
mmiliki huyo kuamua kuregeza kamba na kumuachia mchezaji huyo.
Lakini Samatta aliichezea Simba kabla ya kujiunga na
TP Mazembe mnamo mwaka wa 2011na kisha kutimkia TP Mazembe ya Congo na sasa
huyo nchini Ubelgiji katika klabu yake mpya ya Genk.
Post a Comment