
Klabu ya soka ya Yanga imeahirisha safari ya Afrika
Kusini sasa kubadiri muelekeo wao na kuelekea Tanga kwa ajili ya mchezo wao wa
jumamosi wa Ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Coastal Union.
Mkuu wa kitengo cha habari na mawasiliano cha klabu
ya soka ya Yanga Jerry Muro amesema hawataenda Afrika Kusini na baadala yake
wanaelekea mjini Tanga katika mchezo wao dhidi ya Coausta.
Muro amesema wameamua kwenda Tanga baada ya kunyimwa
kibari na Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF cha kusafiria hivyo wanakwenda
Tanga kwaajili ya mchezo wao huo wa jumamosi.
Klabu ya Yanga ilitaka kwenda Afrika Kusini kwaajili
ya kujiandaa na mchezo wake wa Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Cercle de
Joachim ya Mauritius utakaopigwa Februari 13, nchini Mauritius.
Na hatua hii imekuja baada ya klabu ya soka ya ya
Azam kupewa ruhusa na TFF kuelekea nchini Zambia kwaajili ya kucheza michezo ya
kirafiki kwaajili ya mashindano yao ya kombe la shirikisho.
Post a Comment