
Nahodha wa zamani wa klabu ya mashetani wekundu wa
Manchester United Nemanja Vidic ametangaza rasmi kutundika daruga zake baada ya
kutoka katika klabu ya soka ya Inter.
vidic mwenye miaka 34 hivi sasa alikuwa beki nguli
katika klabu yake ya zamani ya Man u pindi alipokuwa akikutana na timu pinzani.
katika taarifa yake katika mtandao wa United Vidic
amesema muda wake umefika wa kuachana na masuala ya soka na maumivu yote aliyopata
sasa inatosha katika soka.
vidic amesema anawashukuru wachezaji wenzake
aliokuwa anacheza nao,makocha wote walokuwa juu yake ambao alikuwa na anafanya
nao kazi ,wafanyakazi waliokuwa wanashirikiana nae na shukurani kubwa ziene kwa
mashabiki wote wa soka duniani kote ambao walikuwa wanampa sapoti katika mchezo
wa soka kwa miaka yote.
Post a Comment