
Klabu ya soka ya Manchester United, watajitupa
ugenini katika dimba la iPro kuwakabili Derby County, katika hatua ya nne ya
kombe la FA.
Man United watakua na presha kubwa ya mchezo huo
baada ya timu hiyo kutokua na mwenendo mzuri huku kocha wake Luis Van Gaal
akishutumia kwa timu hiyo kuboronga.
Kiungo Michael Carrick huenda akareje katika mchezo
huo baada ya kukosa michezo minne kwa sababu ya majeraha,huku beki Matteo
Darmian akiukosa mchezo huo sambamba na Bastian Schweinsteiger na Phil Jones
ambao pi hawajajumuishwa kwenye kikosi hicho.
Derby wao wapo Nafasi ya 6 kwenye Msimamo wa Ligi
daraja la kwanza (Championship) nao wendo wao si mzuri wakiwa hawajashinda
michezo mitano iliyopita ya ligi.
Post a Comment