Chanongo kushoto na ubwa kulia,picha kwa msaaada wa mtandao wa klabu ya TP Mazembe.
Wachezaji Abuu Ubwa na Haruna Chanongo anayekipiga
katika klabu ya Stand United leo watafanya mazoezi ya majaribio yao katika
kikosi cha TP Mazembe cha DR.
Katika Mazoezi ya leo wachezaji Ubwa ,23, na
Chanongo ,24, ambao wamepata nafasi hiyo ya majaribio wanaweza kuchukuliwa kama
watafuzu majaribio hayo.
Chanongo aliwahi kucheza Simba na Ubwa aliwahi
kukipiga Ureno na Yanga na sasa bahati iko mkononi mwao.
Kwa upande wa Afisa habari wa Stand United Deo Makomba
amesema Uongozi mzima wa Stand United unamtakia majaribio mema mchezaji wao huyo
na endapo atafuzu majaribio hayo wataketi kuzungumza na klabu hiyo juu ya hatma
ya mchezaji wao Chanongo.
Post a Comment