Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

SAKATA LA CHANONGO NA UBWA LAIBUKA UPYA,STAND UNITED YASEMA HAINA TAARIFA YOYOTE JUU YA KUONDOKA KWA WACHEZAJI HAO.



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgoxSiDXAmpFwhR8PSTuzECqNdTENh75hkckjpp7ax2k7yGmPy4k7TDhI_BXEftCKlv8F_7bhGNQ8hV5dnLCDL1A19_xHBOUW00BFNbmEk_KfGGOcLqlfajXeOElYuwwHL1fhmnZRbya5k/s1600/home-1451971605_04ja16-haruna-chanongo-et-abuu-ubwa-zuberi-deux-tanzaniens-a-l-essai-au-tpmazembe_1451971605_1451971605.jpg 
Uongozi wa Klabu ya Stand United ya Shinyanga umeibuka na kudai kuwa hauna taarifa yoyote juu ya kuondoka kwa wachezaji wao Haruna Chanongo na Abuu Ubwa kwenda kufanya majaribio kwenye timu ya TP Mazembe ya Congo DR.


Hivi karibuni wachezaji hao walitimkia katika klabu hiyo ya Congo DR kwa ajili ya kufanya majaribio ya siku 10, zoezi ambalo walilifanya na hatimaye kufanikiwa kufuzu huku hivi sasa wakiwa wanasubiri kauli ya mwisho kutoka kwa mmiliki Moise Katumbi.

Afisa habari wa Stand United Deo Makomba amesema amekuwa akisikia tu kwenye vyombo vya habari juu ya wachezaji hao lakini haina taarifa yoyote rasmi kuhusiana na kuondoka kwa wachezaji ho kwanda kufanya majaribio TP Mazembe.

Akizungumza na Kilowoko.blogspot.com Makomba amesema kocha mkuu wa timu hiyo Patrick Liewig amemwambia kwamba katika meza yake hakuna taarifa yoyote juu ya kutokuwepo kwa wachezaji hao hao.

“Kocha Liewig amenidokeza kwamba anashangazwa na kitendo cha wachezaji hao(Chanongo na Ubwa) kutojitokeza mazoezini kwa kipindi kirefu, tena bila taarifa yoyote,”alisema Makomba.

Uongozi wa Stand unaonekana kuleta sintofahamu kwa sababu hivi karibuni wakala wa wachezaji hao Fadhili Mtemi au Mtaifa alizungumza na Kilowoko.blogspot.com kwa njia ya simu na kukiri kwamba kila kitu kilikwenda sawa na kwamba waliwasiliana na uongozi wa Stand kalbla ya wachezaji hao hawajaenda kuitumikia klabu hiyo kuwa wakipata timu nje lazima klabu hiyo iwaruhusu.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget