Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

SIMBA NAYO YASEMA ITATOA TAMKO SIKU YA KESHO KAMA ITAONDOKA AU LAA.

 

Siku moja baada ya Azam kusafiri kwenda nchini Zambia kucheza mashindano maalum ya mualiko, hatimaye Simba na Yanga nazo zimeamua kufanya ziara zake za mazoezi.

Ligi kuu Tanzania Bara imepumzika kwa muda baada ya mechi za duru la kwanza kumalizika wiki iliyopita huku la pili likitarajiwa kuendelea mwishoni mwa wiki hii.
Wakati Ligi hiyo ikiwa kwenye mapumziko mafupi, michuano ya kombe la FA imekuwa ikiendelea kuchezwa.
Lakini Yanga imeibuka na kudai kwamba ipo mbioni kusafiri kwenda nchini Afrika Kusini kucheza mechi kadhaa za kirafiki ili kujiweka fiti zaidi.
Mkuu wa Kitengo cha habari cha Yanga, Jerry Muro amesikika akisema kwamba wataondoka nchini Ijumaa kwa ajili ya kambi hiyo.
Kambi ya Yanga inatarajia kuwa katika mji wa Johannesburg ambako itaweka kambi inayotarajiwa kuwa ya zaidi ya siku tano.
Kama hiyo haitoshi, kutoka kwa Simba SC kuna taarifa za uhakika zinaeleza kwamba nao wako mbioni kusafiri juma hili kwenda Kenya kwa ajili ya kushiriki mashindano maalum.
 
kwa sasa wanasubiriwa simba kuona je kweli na wao wataondoka nchini kuelekea nchini kenya

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget