Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

SIMBA YAMKANA KIM POLSEN KUFANYA NAE MAZUNGUMZO.



 

Klabu ya soka ya Simba imekanusha kufanya mazungumzo na kocha Kim Poulsen raia wa nchini Denmark kama ambavyo taarifa za awali zilizoripotiwa kuwa klabu hiyo imefanya mazungumzo na kocha huyo ili kuchukua mikoba ya aliyekuwa kocha wao wa zamani Dlyan Kerr raia wa nchini Uingereza baada ya kutimuliwa.


Afisa habari wa Simba Hajji Manara amesema wao kama klabu bado hawajafanya mzungumzo na kocha huyo kama inavyoripotiwa katika vyombo vya habari huku akikiri kufanya mazungumzo na kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Hemed Morocco ambaye walishindwana kutokana na maslai aliyokuwa anataka kocha huyo.

Hata hivyo Manara amesema kwa sasa wanampango wa kuangalia kocha nje ya Tanzania hasa katika bara la Afrika au nje ya bara la Afrika na jitihada hizo zinaendelea kwa haraka zaidi ili kumpata kocha mpya wa klabu hiyo.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget