Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

VIJANA WA KITUO CHA MANYIKA SASA MAMBO MAZURI



                               kijana Said Khalid

 
Mlinda mlango chipukizi Said Khalid Kipao ambaye yupo katika kituo cha kukuzia vipaji vya makipa kilichopo chini ya Mlinda mlango wa zamani wa timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars Peter Manyika anatarajia kuondoka nchini February mosi mwaka huu kuelekea nchini Msumbiji kwaajili ya kufanya majaribio katika klabu ya Quelimane inayoshiriki ligi kuu ya nchini humo.

Akizungumzia safari yake hiyo kijana Saidi amesema anamshukuru mwalimu wake Manyika ambaye ni msaada mkubwa wa safari yake hiyo kwa kumuamini hadi kushawishika kumpeleka nchini Msumbiji na atajitahidi kufata yale aliyoelekezwa alipokuwa kituoni hapo.

Naye Peter Manyika ambaye ni mwalimu wa kituo hicho amesema kijana huyo amepata bahati ya kwenda katika klabu hiyo ambayo inashiriki ligi kuu katika mji wa primeiro de Maio uliopo nchini Msumbiji na ni mategemeo yake atafanya vizuri kulinga na kituo chake kutoa makipa chipukizi wenye viwango vya juu zaidi.



Manyika amesema kabla ya Mwasongwe kwenda nchini Msumbiji lakini pia kuna mlinda mlango mwingine chipukizi kutoka katika kituo chake ambaye nae anaelekea nchini huo siku ya kesho kwaajili ya kufanya majaribio katika klabu nyingine.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget