
Oganaizesheni ya ngumi za kulipwa nchini TPBO
imesema kuwa inaimani na bondia Francis Cheka kuelekea katika pambano lake la
kuwania ubingwa wa dunia dhidi ya bondia Mserbia Ajetovic.
Akizungumza na kilowoko.blogspot.com Rais wa TPBO Yassin Abdallah
amesema pambano hilo linalosubiriwa na wapenzi wengi wa masubwi nchini
linatarajiwa kupigwa February 27 mwaka huu jijini Dar es Salaam na maandalizi
yake yote yamekamilika.
Yassin amesema pamoja na bondia Cheka kutandikwa
hivi karibuni na bondia mwenzake Thomas Mashali lakini si sababu ya bondia huyo
kupoteza ubingwa katika pamabano hilo.
Post a Comment