Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

NAPE AFANYA UTUMBUAJI WA JIPU KWA KATIBU WA BMT,NA NAFASI YAKE KUCHUKULIWA NA SAID KAGANJA.



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgKB0LAGtFdMzyjnkhYpYa2Ad9HShkddmI-uac3kMkXZzO1Al27TUJwvCBMkJYg_y2Je03ZdI_zdSRDMUbFph1QyrctdRmdIeFpBq8Ocrp9EgyNBYFmG0WLvrC-9Aiso5GlTSpUmBRaz6P4/s1600/0635-NAPE+AKIONGEA.jpg 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Wasanii na Michezo, Nape Nnauye ametengua uteuzi wa Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo Tanzania Henry Lihaya baada ya kushindwa kutekeleza wajibu wake.


Mhe. Nnauye alitengua uteuzi huo katika ziara yake aliyoifanya leo mapema katika ofisi za BMT kuona miundo mbinu ya ofisi hizo na kujua changamoto walizonazo.

Aliongeza kwa kusema kuwa, miaka saba ambayo Lihaya amekuwa Katibu Mtendaji wa Baraza imetosha kwani hakuna mabadiliko yoyote aliyoyafanya katika sekta ya michezo tangu alipoteuliwa mwaka 2009.

Baada ya Mhe. Nnauye kufanya utumbuaji huo wa jipu sasa nafasi ya hiyo ya katibu wa BMT imechukuliwa na Said kaganja kuwa kaimu mtendaji mpya.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa BMT Dionis Malinzi amesema uteuzi huo ni kwa mujibu wa sheria ya BMT namba 12 ya 1967 kifungu namba 5(1) baada ya kupata idhini ya Waziri mwenye dhamana. 

UZOEFU WA SAID KIGANJA KATIKA MICHEZO.

kabla ya uteuzi huo Kiganja alikuwa Afisa michezo Mkuu katika ofisi ya Rais,Tawala za mikoa na Serikali za mitaa (TAMISEMI) kuanzia mwaka jana mpaka uteuzi wake leo hii ulipofanyika.

Pia kiganja aliwahi kufanya kazi kama Afisa mwandamizi wa michezo wa Baraza la michezo Tanzania na Afisa michezo Mkuu katika ofisi ya Waziri mkuu.

Kaganja ana shahada ya kwanza ya Elimu katika masuala ya michezo na Utamaduni kutoka katika chuo cha Dar es Salaa.

Aidha, Mhe. Nnauye amemuagiza Katibu Mkuu wa wizara ya habari, utamaduni sanaa na michezo kumpangia Lihaya kazi nyingine ya kufanya wizarani.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget