Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

CHELSEA HOI KATIKA MCHEZO WA JANA WA LIGI YA MABINGWA DHIDI YA PSG



 
Klabu ya PSG kutoka Ufaransa imepata ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Chelsea katika mechi ya mkondo wa kwanza ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya huku Benfica nao wakiilaza Zenit St-Petersburg.


Paris St-Germain walipata bao la kuongoza kupitia kwa mshambuliaji matata wa Sweden Zlatan Ibrahimovic kunako dakika ya 39.

Chelsea walisawazisha katika dakika ya 45 kupitia kwa Mikel Obi lakini Edison Cavan akaitumia dakika ya 78 kuwaumiza Chelsea.

Bao hilo la Mikel ndilo lake la sita kufungia Chelsea katika karibu miaka 10 aliyokaa katika klabu hiyo ya Uingereza.

Bao pekee la Benfica, waliokuwa nyumbani, lilifungwa na Jonas muda wa ziada kutokana na mkwaju wa adhabu uliopigwa na Nicolas Gaitan.

Hilo ndilo bao lake la 25 msimu huu na la 45 kufungia Benfica katika mechi 56 tangu alipojiunga nao akitokea Valencia mwaka 2014.

Zenit walisalia wachezaji kumi uwanjani baada ya Domenico Criscito kupewa kadi ya pili ya njano dakika ya 90.

Mechi zingine mbili zitapigwa usiku wa leo ambapo…

KAA Gent   vs   VfL Wolfsburg

Roma  vs    Real Madrid

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget