Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

MSANII JOHN WOLKER AANGWA LEO NA MAZISHI YAKE KUFANYIKA MJINI TANGA.



 
Mamia ya watu wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya leo wamejitokeza kwenye hospitali ya Muhimbili kumuaga marehemu Michael Mhina maarufa kama John Walker aliyefariki dunia Jumanne jijini Dar es salaam.

Walker ameagwa mchana wa leo na kisha mwili wake kusafirishwa kwenda jijini Tanga kwa ajili ya maziko.

Msanii huyo alifariki dunia baada ya kulipukiwa na mtungi wa gesi wakati akiutengeneza.

Inaelezwa kuwa mtungi huo wa gari ulilipuka na baadhi ya vipande vya chuma vikamjeruhi kichwani na kumfanya akimbizwe hospitali ya Muhimbili na huko ndiko mauti yalipomkuta.
Msanii huyo kutoka katika kundi la muziki la Watukutu alikuwa maarufu kutokana na kuimba mistari yenye ujumbe lakini kwa sauti ya mlevi.

Ndugu, jamaa na marafiki wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya wamepta fursa ya kumuelezea marehemu John Walker.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget