
KLABU ya soka ya Manchester United imekataa kuzungumzia lolote juu ya kufanya mazungumzo na mawakala
wa aliyekuwa kocha wa Chelsea Jose Mourinho.
Kulikuwa na taarifa kuw klabu hiyo imeshafanya
mzungumzo na kocha huyo kuchukua nafasi ya kocha wa sasa Lous Van Gaal, ambaye anatarajiwa
kuondoka baadaye mwakani.
Maafisa wa juu wa Man United wanatarajiwa kutoa jibu
lao baada ya majirani zao Manchester City kuchukua huduma za Pep Guradiola,mapema
wiki hii.
Na kama Mourinho ataifundisha Man U basi wazi kabisa
kutakuwa na upinzani mkali kati ya City na United kufuatia ule uliokuwepo kati
ya Real Madrid na Barcelona wakati makocha hao walipokuwa katika timu hizo
mbili.
United ambao wakombele dhidi yay a Chelsea ambap klabu
hizi zinatarajiwa kuvaana siku ya jumapili.
Post a Comment