Na Godfrey Mbai
Watani wa jadi katika soka la Bongo Yanga na Simba
wanakutana jumamosi hii katika mechi inayosubiriwa kwa hamu kote nchini ya
mzunguko wa pili wa Ligi kuu Bara.
Tayari joto na presha ya mechi hiyo imeanza kupanda
tangu wiki mbili zilizopita huku kila upande ukijinadi kuibuka na ushindi
katika mechi hiyo yenye kutawaliwa na vituko vya kila aina ndani na nje ya
uwanja.
Kuelekea katika mtanang’e huo Shirikisho la soka
nchini(TFF),mwanzoni wa wiki hii liliweka wazi viingilio vya mechi hiyo huku
kile cha chini kikiwa ni shilingi elfu saba.
Viingilio vingine ikiwa ni kama vile ,kiingilio cha juu cha mchezo huo ni
shilingi Elfu Thelathini (30,000) kwa VIP A, Elfu Ishirini (20,000) VIP B &
C, Elfu Kumi (10,000) kwa vile vya rangi ya machungwa (Orange), na Elfu Saba
(7,000) kwa viti vya rangi ya bluu na kijani.
Katika makala hii tutaangalia ni kwa namna gani mechi
hii inafanya kiingilio cha elfu saba kukubalika miongoni wa wadau wa soka
nchini kuwa kiingilio cha chini kabisa katika mechi hiyo huku mechi nyingine
zikiwa na viingilio vya chini vya
kawaida zikiwemo zile zinazohusisha Yanga na Simba dhidi ya timu
nyingine tofauti na zinapokutana zenyewe.
Ukongwe
wa timu hizo
Hakuna ubishi ata mtoto wa miaka kumi anajua kuwa
Yanga na Simba ndio timu kongwe na zilizodumu kwa muda mrefu katika soka la
Bongo licha ya changamoto za hapa na pale.Yanga ikizaliwa 1935 huku Simba
yenyewe ikisimama 1936 kwa kupita katika
majina kadhaa kama vile Sunderland na kadhalika.
Ukongwe wa timu hizi na idadi kubwa ya mashabiki
walionao unafanya kiingilio cha chini
cha elfu saba au ata elfu15 kukubalika
kirahisi na mashabiki kujitokeza kuwatazama wakongwe hao.
Ukubwa
wa mechi na nafasi za timu hizo katika msimamo wa ligi
Hii inaweza kuwa sababu nyingine ambayo inapekea Tff
kufanya kiingilio cha chini kuwa shilingi elfu saba au zaidi nab ado kukubalika
na wapenzi wa timu hizo nchini na kujitokeza kwa wingi uwanja wa Taifa.
Licha ya kuwa na wakati mgumu chini ya kocha Kerr
Simba wanaingia katika mechi ya jumamosi dhidi ya Yanga wakiwa kileleni mwa
msimamo(shukrani kwa mabadiliko ya ratiba),wakiwa na alama 46 baada ya mechi 19
huku Yanga wakiwa nafasi ya pili na alama 42
katika mechi 18.
Hivyo mashabiki watakua na shauku ya kufika Taifa
ili kujua kama Yanga watapata alama tatu na kuifukuzia Simba au Mnyama ata pata
alama tatu au moja na kuendelea kusalia
kileleni huku wakisubiri Yanga na Azam wacheze viporo vyao?,hapa washabiki
hawana namna zaidi ya kukubali elfu saba au zaidi kama kiingilio cha chini ili
tu kupata burudani na kujua hali ilivyo kimsimamo kwa timu hizo katika ligi.
Hakuna
mechi nyingine yenye kuvuta hisia za wapenda soka nchini
Licha ya Azam kuonekana kuleta upinzani dhidi ya
vigogo ,ukweli unabaki wazi kuwa pambano kati ya wakongwe hawa linabeba hisia
za wapenda soka kote nchini.
Kuanzia viongozi,wanachama na mashabiki wa pande
zote mbili huwa katika vihoro kabla na baada ya mechi hiyo.
Vyombo vya habari ndio usiseme,wiki mmoja kabla ya
mechi magazeti,televisheni,radio na mitandao mbalimbali ya kijamii hutawaliwa
na taarifa za Yanga na Simba, na ata baada ya mechi kwisha mengi husemwa na
kuandikwa juu ya pambano hilo,kwanini usiweke elfu saba au zaidi ya hapo kuwa
kiingilio cha chini wakati kuna mechi mbili tu katika msimu mzima wa ligi kuu
zenye kuvuta hisia nazo ni Yanga na Simba au Simba na Yanga(nyumbani na Ugenni).
Matokeo
ya mechi iliyopita
Septemba mwaka jana katika mechi ya mzunguko wa
kwanza Yanga ilipata ushindi wa 2-0 dhidi ya watani zake
Simba katika dimba la Taifa.Magoli ya Amis Tambwe na Malimi Busungu yalitosha
kupeleka furaha Jangwani na kupeleka huzuni Msimbazi.
Matokeo haya ya mechi ya kwanza yanawapa viburi
mashabiki wa Yanga hivyo kwao inakua rahisi kujitokeza uwanjani wakiamnini timu
yao itaendeleza ubabe huku wale wa Simba wakipata nguvu na matokeo ya siku za
karibuni ya timu yao chini ya kocha Mayanja, hivyo kupata kiburi cha kwenda
Taifa wakiwa na imani ya kupata ushindi.Hapa elfu saba au 15 kama kiingilio cha
chini kabisa bado watu watajaa wa pande zote mbili kila upande ukiamini kuibuka
kidedea.
Kuimairishwa
kwa ulinzi
Kati ya mechi za ligi kuu Bara ambazo ulinzi
uimarishwa na vyombo husika basi hii ya Simba na Yanga ulinzi huwa wa hali ya
juu kwa upande wa watu na mali zao ndani nan je ya uwanja.
Vikosi vya kulinda usalama na kutuliza ghasia
umwagika kwa wingi katika dimba la taifa ndani na nje kwa lengo la kuhakikisha
kuwa kila kitu kinakwenda sawa.
Watu wa Msalaba Mwekundu huwa tayari kutoa huduma
popote pale ndani ya uwanja na nje pindi tatizo linapotokea.
Ata jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Daressalaam
lilisikika likigusia juu ya hali ya kuimarishwa kwa ulinzi na usalama kuelekea
mechi hiyo.
Hapa kwa mpenzi wa soka ni rahisi kukubali kiingilio
cha chini kuwa elfu saba au kumi na tano kwa kuwa tu kuna uhakika wa usalama wa
yeye na mali zake siku ya mchezo,hapa
ndipo Tff wanacheza na akili za watanzania
na kuamini wataenda tu katika dimba la Taifa kutazama mchezo huo.
Mwandishi
wa Makala ni Mtangazaji wa zamani wa kipindi cha Anga za Michezo cha Radio SAUT
Fm.Mwandishi mchangiaji katika magazeti mbalimbali kama vile Kiongozi,Habari
Leo,Jamhuri,Mwanaspoti,Mbiu ya Jamii na Mdadisi.Pia aliwai kufanya kazi kwa mda
mchache katika Radio ya ABM ya Abdallah Majura. Kwa sasa ni mfanyakazi katika
kampuni ya Choice Int’l Forwarding Co,Ltd.
Post a Comment