
Timu za soka za Taifa ya vijana umri chini ya miaka 14
na 17 inatarajia kuingia kambini mapema mwezi huu kwa ajili ya kujiandaa na
mashindano mbalimbali ya vijana.
Akizungumza na KILOWOKO.BLOGSPOT.COM Mkurugenzi wa ufundi
kutoka Shrikisho la soka nchini Tanzania Salum Madadi ameseme vijana hao
wanatarajiwa kuingia kambini muda wowote kuanzia hivi sasa na tayari
wameshaandaa bajeti kwa ajili ya timu hiyo.
Ikumbukwe kuwa timu hiyo ilishindwa kuendelea na
kambi yake ya kila mwezi na kushindwa kuendelea na ziara yake ya nje ya nchi
baada ya TFF kudaiwa kuwa haijalipa kodi kwa muda mrefu na kwa mamlaka ya
mapato nchini TRA.
Post a Comment