
RAIS wa zamani wa Shirikisho la Soka Duniani-FIFA,
Sepp Blatter ameapa kuwa atakubali hatma yake katika maamuzi yatayotolewa na
Mahakama ya Kimataifa ya Michezo-CAS juu ya rufani yake kupinga kufungiwa miaka
sita kujishughulisha na masuala ya soka.
Akihojiwa nje ya ofisi za makahama hiyo huko
Lausanne, Uswisi, Blatter mwenye umri wa miaka 80 amesema takubaliana na uamuzi
wowote utakaotolewa.
Blatter aliongeza kuwa ana matumaini uamuzi
utakaotolewa utakuwa mzuri kwa upande wake lakini akiwa kama mwanasoka amejifunza
kuwa kuna kushinda na wakati mwingine kushindwa pia.
Rais huyo mkongwe alikumbwa na adhabu hiyo kutoka
FIFA kufuatia kukutwa na hatia ya kufanya malipo ya dola milioni mbili kwenda
kwa rais wa zamani wa Shirikisho la Soka la Ulaya-UEFA Michel Platini mwaka
2011.
Post a Comment