Timu ya Taifa ya soka la ufukweni Beach Soccer
ijumaa hii inatarajia kushuka dimbani kukipiga dhidi ya Ivory Cost katika
mchezo wao wa kusaka tiketi ya kufuzu kucheza fainali za kombe la mataifa ya
Afrika.
Mchezo huo utachezeshwa na waamuzi kutoka Uganda
ambao ni Shafic Mugerwa katikati na wasaidizi wake ni Ivan Bayige Kintu na
Muhammad Ssenteza.
Mtunza muda katika mchezo huo atakuwa Adil Ouchker
wa Morocco huku Kamishna akiwa ni Reverien Ndikuriyo wa Burundi.
Timu hizo zinatarajiwa kucheza mechi mbili ambako
mara baada ya mchezo wa Dar es Salaam, utarudiwa mwingine huko Ivory Coast na
mshindi wa jumla atakuwa amefanikiwa kufuzu kwa fainali.
Kikosi hicho kinaunda na wachezaji Talib Ame, Ahamada, Mohammed Makame, Ahamed Rajab (golikipa)
Khamis Said na Yacob Mohamed wote kutoka Zanzibar.
Wengine ni Ally Raby, Mwalimu Akida, Khalifa Mgaya,
Rolland Revocatus, Juma Sultan, Rajab Ghana, Samwel Salonge, Kashiru Salum,
Juma Juma na Kevin Baraka.
Post a Comment