
Kamati ya ufundi ya Shirikisho la soka nchini
Tanzania TFF imeendelea kuhakikisha soka la kitanzania linazidi kupata waalimu
wa kutosha walio na elimu ya kutosha na kuliwezesha soka la kitanzania kuwa la
kimataifa.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa ufundi wa TFF Salumu
Madadi wakati akiendelea kusimamia kozi ya Utimamu wa mwili inayowahusisha
makocha mbalimbali hapa nchini.
Akizungumza na Kilowoko.blogspot.com Madadi amesema kozi
hiyo imelenga zaidi kuwapa walimu hao elimu ya kutosha kuhusu wachezaji ambao
mara zote ndio wao wanaowafundasha baada kuwepo kwa uwingi wa wachezaji
waliomaliza soka lao wakipata magonjwa mbaimbali.
Amesema kigezo walichotumia katika kuendeleza kozi
hiyo ni walimu wote wenye leseni ya daraja B ya ukocha na hii itawafanya kuwa
katika hali nzuri wakati wa kufundisha.
Post a Comment