
Klabu ya soka ya Simba inatarajiwa kuelekea Mjini
Dodoma wikiendi hii kwa ajili ya kucheza mchezo wake wa kirafiki dhidi ya timu
ya Polisi Dodoma inayoshiriki Ligi daraja la Kwanza.
Mbali na kucheza mchezo huo wa kirafiki lakini pia
klabu ya Simba itatumuia mchezo huo kwa lengo la kusapoti kauli ya Rais wa
Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Magufuli ya kuanza harakati za kuhamia
mjini humo.
Akizungumza na waandishi wa habari Msemaji wa klabu
ya soka ya Simba HAJJI MANARA amesema watatumia mchezo huo kwa ajili ya kucheza
na klabu hiyo na kuwafundisha soka safi lakini pia kuunga mkono kauli ya Rais
Magufuli ya kuhamia Dodoma.
Post a Comment