Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

TWIGA STARS KUANZA NA ETHIOPIA NA RWANDA CHALLENGE.



Image result for TWIGA STARS 
TIMU ya Taifa ya soka la wanawake ya Tanzania Twiga Stars imepangwa Kundi B pamoja na Ethiopia na Rwanda katika michuano ya ubingwa wa wanawake kwa mataifa ya Afrika Mashariki na Kati. 

Msemaji Mkuu wa TFF Alfred Lucas amesema kuwa utambulisho wa michuano hiyo ya Challenge kwa upande wa wanawake ilifanyika jana mjini kampala, wenyeji wa michuano iyo watakuwa ni nchi ya Uganda.

Amesema timu hiyo itakuwa na kambi yake katika Hosteli za karume kwa muda wa wiki moja kabla ya kufanya kambi ya muda mrefu kujiandaa na michuano hiyo.

Mbali za Tanzania, Ethiopia na Rwanda Kundi A linaundwa na timu za Uganda, Kenya, Burundi, na Zanzibar na michuano itaanza Septemba 11 hadi 20, 2016.

Kwa upande mwingine Lucas ameelezea kuendelea kwa timu ya Taifa Stars na mazoezi yake wakijiweka sawa kwa ajili ya mchezoi wake dhidi ya timu ya Nigeri utakaopigwa Septemba 3 mwaka huu.

Lucas hakuishia hapo ameelezea pia kuingia kambini kwa timu ya Tifa ya vija ya Serengeti Boys ambayo inatarajiwa kuingia kambini jumatano hii kabla haijaelekea nchini Shelisheli kwa ajili ya kuweka kambi ya muda mrefu zaidi.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget