
KIUNGO wa Arsenal, Jack Wilshere anatarajiwa
kujiunga na Crystal Palace au Bournemouth kwa mkopo wa msimu mzima ili aweze
kupata nafasi ya kucheza katika kikosi cha kwanza.
Nyota huyo mwenye umri wa miaka 24 amekutana na
meneja wa Palace, Alan Pardew na yule wa Bournemouth Eddie Howe jana kwa ajili
ya mazungumzo.
Wilshere ameichezea Uingereza mechi sita katika
kipindi cha kiangazi zikiwemo mechi tatu za michuano ya Ulaya lakini ameachwa
katika kikosi cha nchi hiyo kinachoongozwa na kocha mpya Sam Allardyce.
Post a Comment