Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

KLABU YA SIMBA KUKIPIGA KESHO DHIDI YA POLISI DODOMA.



Image result for WEKUNDU WA MSIMBAZI 
Mashabiki wa klabu ya soka ya Simba wameelezea furaha yao juu ya uimara wa kikosi chao cha wekundu wa msimbazi  kuwa bora zaidi kuliko timu nyingine kwa msimu huu mpya wa ligi kuu soka Tanzania bara na kujihakikishia lazima kitatwaa ubingwa wa ligi hiyo.

Mashabiki hao wamesema kutokana na usajili uliofanya na uongozi wao kwa kuwaleta wachezaji waliona uwezo wa kusakata kabumbu ni wazi kuwa ligi ya msimu huu kwa upande wao ni mchekea tuu.

Klabu ya soka ya Simba jumamosi hii inashuka dimbani kukipiga dhidi ya timu ya polisi Dodoma inayoshiriki ligi daraja la kwanza ukiwa ni mchezo wa kirafiki lakini pia ni kuunga mkono kauli ya Rais Mhe.Dkt John pombe Magufuli juu ya kuhamia mjini Dodoma kwa Wizara nyeti za Serikali.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget