Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

MAJIMAJI YATANGAZA HALI YA HATARI KWA SIMBA KUELEKEA KATIKA MCHEZO WAO WA KESHO.



Image result for KLABU YA MAJIMAJI 
Timu ya soka ya Majimaji FC ya Songea imetangaza hali ya hatari kwa wekundu wa msimbazi Simba ambao Jumamosi hii watacheza mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Mjumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo Salum Msamaki amesema wanaamini kikosi chao kitakua cha kwanza kwa msimu huu kuifunga timu ya Simba ambayo inaongoza msimamo wa ligi ikiwa haijapoteza mchezo hata mmoja kwa msimu huu wa 2016/17.

Wakati huohuo suala la ukata ndani ya klabu ya Majimaji FC huenda likafikia kikomo siku kadhaa zijazo, kufuatia neema ya udhamini inayoinyemelea klabu hiyo kongwe huko mkoani Ruvuma.

Salum Masamaki amesema wamekua na mazungumzo na kampuni ya GSM ambayo imeonyesha dhamira ya kweli ya kuwekeza ndani ya Majimaji FC.

Amesema endapo mambo yatakamilishwa kama wanavyotarajia, kikosi chao kitakua na kila sababu ya kufanya vizuri katika michezo inayowakabili na huenda wakamaliza kwenye nafasi nzuri katika msimamo wa ligi kuu msimu huu.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget