Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

MARTINEZI AWATAKA MASHABIKI WA UBELGIJI WASITEGEMEE MCHEKEA KWA MUDA MFUPI.



Image result for MARTINEZ 
KOCHA mpya wa timu ya taifa ya Ubelgiji, Roberto Martinez ameanza vibaya kibarua chake hicho baada ya kuchapwa mabao 2-0 katika mechi ya kwanza dhidi ya Hispania na kujikuta akizomea na mashabiki waliojitokeza kushuhudia mchezo huo.

Martinez raia wa Hispania mwenye umri wa miaka 43, aliteuliwa kushika nafasi hiyo Agosti 3 mwaka huu ikiwa imepita miezi mitatu toka atimuliwe Everton.

Akihojiwa kuhusiana na hilo, Martinez amesema ni jambo lisilowezekana kutegemea mabadiliko makubwa katika kipindi kifupi hivyo mashabiki wanapaswa kuwa na subira.

Katika mechi zingine za kirafiki za kimataifa zilizochezwa jana, Ufaransa ilifanikiwa kuichapa Italia mabao 3-1, Ugiriki ikiichapa Uholanzi kwa mabao 2-1 wakati mabingwa wa Ulaya Ureno wakiiburuza Gibraltar kwa mabao 5-0.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget