Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

KIPIGO CHA STARS MKWASA AFUNGUKA ETI NAYO TFF NI CHANZO KUMBE.



Baada ya kuwasili nchini kwa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars, Kocha Mkuu wa timu hiyo Charles Boniface Mkwasa amefunguka na kuelezea kilichowasibu wao kupoteza mchezo wao dhidi ya timu ya Taifa ya Nigeria katika mchezo wa  kumaliza kukamilisha ratiba ya kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa Afrika.

Mkwasa amesema kutojipanga vyema kwa Shirikisho la soka nchini Tanzania TFF kumechangia kwa kiasi kikubwa timu hiyo kutofanya vyema katika mchezo wake huo kutokana na kutawala kwa siasa nyingi za kukosa fedha kwa TFF hali inayosababisha timu hiyo kutoweza kuwa na programa ya mazoezi kwa wakati unaotakiwa.Image result for mkwasa


Mkwasa hakuishia hapo pia alielezea misukosuko ya safari yao na hii inasababishwa na kutokuwa makini kwa TFF na kutojiandaa vyema kumesababisha hata katika safari yao kuwepo kwa mizengwe mingi kutokana na wasafirishaji wao kushindwa kuwapa huduma nzuri kwa wakati unaotakiwa.

Kwa upande mwingine Mkwasa amegoma kupewa kwa Adhabu kwa beki kisiki Kelvin Yondani kwa kuonyesha utovu wa nidhamu wa kutosafiri na timu na kuelezea kwa upande wake haoni kama inamaana ya kumpa adhabu bali ni TFF kuhakikisha wanaongeza motisha kwa wachezaji wa timu ya Taifa.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget