Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

ZLATANI AMNUSURU MOURHINHO.



Image result for ZLATAN IN MAN U 
Manchester United wameondoka kwenye mkia katika kundi lao la ligi ndogo ya Ulaya, Europa League, baada ya kupata ushindi dhidi ya Zorya Luhansk.
Zlatan Ibrahimovic alifunga bao la pekee dakika ya 69, baada ya kombora la nguvu mpya Wayne Rooney kugonga mlingoti wa goli.

Hilo ndilo bao la kwanza la Ibra katika mechi tano, na lilitokana na kombora la kwanza la United lililolenga goli kwenye mechi hiyo.

Mashetani hao Wekundu walitarajiwa kufanya vyema Europa League lakini walianza kampeni yao kwa kulazwa 1-0 na klabu ya Feyenoord ya Uholanzi mechi yao ya kwanza.

United sasa wamo katika nafasi ya tatu katika kundi lao wakiwa na alama sawa na Feyenoord na moja nyuma ya viongozi Fenerbahce wa uturuki ambao watazuru Old Trafford 20 Oktoba.

United watarejea uwanjani Jumapili Ligi ya Premia ambapo watacheza dhidi ya Stoke City dimba la Old Trafford

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget