Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

MBEYA CITY USO KWA USO NA STAND UNITED.



Image result for MBEYA CITY 
KIKOSI cha Mbeya fc  kinatarajia kushuka kwenye uwanja wa Sokoine jijini Mbeya hapo kesho(Ijumaa) kucheza mchezo mwingine muhimu wa ligi kuu ya soka Tanzania bara dhidi ya wageni Stand United  kutoka mkoani Shinyanga kikiwa bila nyota wake kadhaa wa safu ya ulinzi.

Kwa mujibu wa  Ofisa  habari, Dismas Ten, maandalizi kuelekea  mchezo huo yamekamiliki na City itashuka dimbani ikiendelea kuwakosa nyota wake wawili wa safu ya ulinzi, Haruna Shamte na Sankhani Mkandawile ambao walimua  kwenye mchezo wa ugenini dhidi ya JKT  Ruvu uliochezwa Mlandizi mkoani Pwani na City kufungwa bao 2-0.

Katika  Hatua  nyingine nahodha wa Mbeya City Fc , Kenny Ally   ameipogeza  timu ya taifa ya vijana Serengeti Boys kwa hatua nzuri waliyofikia licha ya kushindwa kufuzu kwa michuano ya Afrika baada ya kufungwa bao la dakika za lala salama  kwenye mchezo wao wa mwisho huko nchini Congo.

Kenny Ally ambaye alikuwa mmoja wa nyota wa timu ya taifa ya Tanzania waliokwenda nchini Brazil na kutwaa kombe la Copa Coca cola licha ya kutoa pongezi wa shirikisho pia alitoa wito kwa rais Jamal Malinzi kuhakikisha anaitunza vyema timu hii ili ije kuwa timu nzuri ya taifa siku za usoni.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget