Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

HAPA THOMAS MASHALI PALE FRANCIS CHEKA HAPATOSHI KESHO KATIKA UWANJA WA JAMUHURI.



 

Na Merina Robert
Morogoro


MABONDIA Francis Cheka bingwa wa ngumi za kulipwa dunia wa uzito wa kati(WBF) na mwenzake Thomas Mashali kila mmoja ametamba kumpiga mwenzake  katika pambano lisilo na ubingwa linalotarajia kufanyika siku ya sikukuu ya Kristimas Desemba 25 katika uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro.
Wakizungumza mara baada ya kupima uzito mabondia hao  katika kituo cha mabasi Msamvu ambapo mabondia  wote walikutwa na uzito wa kilo 77 bondia Francis Cheka amesema amejiandaa vizuri na kwamba hawezi kuzungumza zaidi anasubiri ulingoni huku bondia Thomas Mashali akisema kuwa naye amejiandaa vizuri hivyo haogopi kupambana na bondia mwenye jina.
Kwa upande wake mmoja wa mabondia wanawake anayetarajia kucheza kwenye pambano la Utangulizi  Lulu Kayage  na bondia mwenzake wa kike Mwanne Haji amesema kuwa mabondia wanawake wamekuwa wakisahauliwa na mapromota katika mapambano mbalimbali licha ya kuwa na uwezo mkubwa kwenye mchezo huo na kuahidi kufanya vizuri kwenye pambano lake.
Naye mwandaaji wa pambano hilo Siraji Kaike amesema pambano hilo litakuwa na ushindani mkubwa kutokana na mabondia wote kujiandaa vya kutosha na kwamba matokeo yoyote yanaweza kutokea .


Katika pambano hilo litatanguliwa na mapambano ya utangulizi baina ya mabondia Deo Njiku na  Vicent Mbilinyi,lulu Kayage na  Mwanne Haji,Seba Temba na Pius Kazaura,Twaha Kiduku na Ibrahim Clasic,Mohamed Matumla na Kudra Tamimu,Epson John na Sadick Momba na Mfaume Mfaume na Kasim Mohamed.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget