Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

SAKATA LA OKWI LA RUDI TENA,SASA SIMBA YAIPIGA MKWARA ETOILE DU SAHEL.



 

Uongozi wa klabu ya soka ya Simba umeitaka klabu ya soka ya Etoile Due Sahel ya nchini Tunisia kuhakikisha wanailipa klabu hiyo mapema fedha za aliyekuwa mchezaji wao Emmanuel Okwi  kabla ya kufikia mwezi March mwakani.


Akizungumza na waandishi wa habari msemaji wa klabu hiyo Haji Manara amesema klabu hiyo ya Etoile Due Sahel iliandika barua kwenda Shirikisho la soka Dunia FIFA kutaka kuongezewa muda wa kulipa deni lao ndani ya klabu ya Simba Mwezi March mwakani jamabo ambalo uongozi wa Simba umepinga suala hilo.

Klabu ya Simba inaidai klabu ya Etoile Du Sahel takrimbani sh. milioni 600 kwaajili ya mchezaji wao Emmanuel Okwi ambazo hazijalipwa hadi sasa nadani ya klabu hiyo.

Okwi alinunuliwa na Etoile Januari mwaka 2013 kwa dau la dola 300,000sawa sawa na shilingi Milioni 600 za kitanzania ingawa baada ya muda akaingia kwenye mgogoro na klabu hiyo ya Tunisia.

Mtafaruku ulianza baada ya Okwi kuchelewa kurejea mjini Sousse mkoani Sahel baada ya ruhusa ya kwenda kuichezea timu yake ya taifa, Uganda.

Okwi naye akadai Etoile walikuwa hawamlipi mishahara na kufungua kesi FIFA (Shirikisho la Soka la Kimataifa), ambayo mwisho wa siku alishinda kwa kuruhusiwa kutafuta timu nyingine ya kuchezea kulinda kipaji chake, wakati wa mgogoro wake na klabu ya Tunisia.

Hata hivyo, Okwi  mapema Oktoba mwaka huu, Simba SC nayo ilimuuza katika klabu ya SonderjyskE FC inayoshiriki ya Ligi Kuu ya Denmark ambako amesaini Mkataba wa miaka mitano.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget