Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

ARSENAL WATAKATA KOMBE LA FA.



Image result for theo walcott 
Klabu ya soka ya Arsenal imefika robo fainali ya Kombe la FA baada ya kuilaza Sutton United kupitia mabao ya Lucas Perez na Theo Walcott.

Katika mechi hiyo iliyochezewa Gander Green Lane, Wenger alifanya mabadiliko saba katika kikosi kilichochapwa 5-1 na Bayern Munich mechi ya mkondo wa kwanza hatua ya 16 bora katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya wiki iliyopita.

Kikosi chake kilikuwa an nguvu za kutosha kuwazidi wapinzani hao ambao wamo nafasi 105 chini yao katika orodha ya ustadi wa klabu Uingereza.
Lucas Perez alifungia Arsenal bao la kwanza dakika ya 26 naye Theo Walcott akaongeza la pili dakika 10 baada ya kipindi cha pili kuanza.

Ushindi huo ulimpunguzia shinikizo meneja Arsene Wenger na Arsenal sasa watakutana na Lincoln City katika robo fainali ukizingatia Lincoln walifika robo fainali kwa kuwalaza Burnley Jumamosi.

Mchezo mwingine unaosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa soka ni ule kati ya Chelsea na Man U ambao wanatarajia kukutana robo fainali FA.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget