Mlinda mlango wa klabu ya soka ya
Arsenal Peter Cech amesema klabu yake inaweza ika twaa ubingwa wa ligi kuu soka
nchini Uingereza kwa sababu ya kurejea kwa wachezaji wake wengi waliokuwa
katika majeraha.
Cech
amesema baada ya kurejea kwa wachezaji wengi wa klabu hiyo walio majeruhi wanaweza
wakatwaa ubingwa wa ligi kuu nchini Uingereza.
Washika
mitutu hao wa jiji la London waliwatandika Manchester City mabao 2-1 katika
dimba la uwanja wa Emirates siku ya Jumatatu kwa ushindi huo sasa inamaanisha
wameshinda michezo 11 kati ya 17 waliokwishacheza ya ligi hiyo.
Vijana hao wa Mzee Arsene Wenger's wameshinda michezo yote hiyo bila ya wachezaji wake hatari Jack Wilshere, Mikel Arteta, Santi Cazorla, Danny Welbeck, Tomas Rosicky na Francis Coquelin.
Mlinda mlango huyo Peter Cech anaamini baada ya kurejea kwa wachezaji wote hao waliomajeruhi wanaweza wakatwaa ubingwa wa ligi hiyo ifikapo mwezi May mwakani.
Vijana hao wa Mzee Arsene Wenger's wameshinda michezo yote hiyo bila ya wachezaji wake hatari Jack Wilshere, Mikel Arteta, Santi Cazorla, Danny Welbeck, Tomas Rosicky na Francis Coquelin.
Mlinda mlango huyo Peter Cech anaamini baada ya kurejea kwa wachezaji wote hao waliomajeruhi wanaweza wakatwaa ubingwa wa ligi hiyo ifikapo mwezi May mwakani.
Post a Comment