Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

PELLEGRINI AJITAPA KUWASAMBALATISHA SUNDERLAND LEO.



City 

Yakiwa yamesalia masaa machache kuwa vaa Sunderland Meneja wa Manchester City Manuel Pellegrini amesema anaamini timu yake ndiyo yenye nguvu zaidi katika Ligi kuu soka nchini Uingereza kutokana na kutokuwa na wachezaji wengi walio majeruhi.


City kwa sasa wanashika nafasi ya 3 katika ligi wakiwa na alama sita nyuma ya vinara Leicester baada ya kutandikwa mabao 2-1 na Arsenal Jumatatu ya wiki hii.

Nahodha wao Vincent Kompany, 29, anatarajiwa kurejea kikosini baada ya kukosa mechi tisa. Huku Mshambuliaji wao Sergio Aguero naye amekosa michezo 11 kutokana na jeraha na akitarajiwa kurudi dimbani.

Ukiachana na wachezaji hao lakini nae beki wao Pablo Zabaleta na kiungo wa kati Fernando pia wanatarajiwa kurejea baada ya kuuguza majeraha yaliyokuwa yanawasumbua kwa muda mrefu.

City walifanikiwa kumaliza mechi saba bila kufungwa Ligi Kuu ya Uingereza wakiwa na Kompany lakini baada yake kuumia, wamefanikiwa kumaliza mechi moja pekee kati ya sita bila kufungwa goli.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget