Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

NEYMAR AZIDI KUANDAMWA NA MAJANGA.



 

Waendesha mashtaka nchini Brazil wamependekeza kwamba nyota wa timu ya Barcelona Neymar ashtakiwe na mashtaka matatu ya ufisadi kuhusu kesi ya kodi wakati wa uhamisho wake hadi Barcelona.


Inadaiwa kwamba kampuni zilibuniwa ili kutumika kwa niaba yake ili mchezaji huyo alipe kodi ya kiwango cha chini.

Maafisa nchini Brazil wanasema kuwa madai hayo dhidi ya mshambuliaji huyo wa Barcelona yanasimamia kipindi cha miaka saba kuanzia 2006.

Madai hayo ni tofauti na yale ya kesi iliosikizwa siku ya Jumanne nchini Uhispania.

Neymar alihudhuria kesi yake ya madai ya ufisadi kuhusu uhamisho wake na Amekana kufanya makosa yoyote.

Madai hayo ya viongozi wa mashtaka yatakwenda kwa jaji ambaye ataamua iwapo kuna kesi ya kujibu au la na kwa sasa Neymar sio mshtakiwa.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget