Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

MADRID WAGANDWA NA DORTMUND MICHUANO YA LIGI YA MABINGWA.



Image result for karim benzema 
KLABU ya Real Madrid imefikia rekodi ya kutofungwa mechi 34 kufuatia sare ya mabao 2-2 dhidi ya Borussia Dortmund katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya jana.

Hata hivyo, matokeo hayo hayakutosha kuifanya Madrid kufuzu hatua ya timu 16 bora wakiwa vinara wa kundi F baada ya kuzidiwa na wapinzani wao Dortmund.

Madrid walionekana kumudu vyema mchezo kufuatia mabao mawili mawili yaliyofungwa na Karim Benzema lakini mambo yalibadilika baada ya mabao ya kusawazisha Pierre-Emerick Aubameyang na Marco Reus.

Kipigo chao cha mwisho kilikuwa ni mabao 2-0 walichopata kutoka kwa Wolfsburg katika michuano hiyo Aprili 6 msimu uliopita na toka wakati huo wamepata ushindi katika mechi 24 na kutoa sare tisa katika mashindano yote huku wakifunga mabao 94 na kuungwa 31 pekee.

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget