Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

MCHEZO WA MBAO NA KAGERA SUGAR WAHAHIRISHWA KUPISHA SHUGHURI ZA KISERIKALI



Image result for KLABU YA MBAO FC 
Mchezo wa kirafiki uliokuwa ufanyike hii leo kati ya Mbao FC na Kagera Sugar kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza umehairishwa kutokana na kuingiliana kwa matumizi ya uwanja.

Afisa habari wa klabu ya Mbao fc Krisanti Malinzi amesema kuwa mchezo huo ulitakiwa ufanyike siku ya leo lakini kutokana na Serikali kutaka kuutumia uwanja wa CCM kirumba imewabidi kuhairisha mchezo wao huo.

MALINZI amesema kuwa mchezo huo ulikuwa maalumu kwa ajili ya kutoa heshima kwa marehemu Ismail Khalfan - mchezaji wa timu ya vijana ya Mbao aliyefariki dunia Desemba 4, mwaka huu wakati akiiitumikia timu yake ya vijana kwenye mchezo wa Ligi ya Vijana ya TFF U20 dhidi ya Mwadui, uliofanyika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba, Kagera.

Kadhalika, mchezo huo utatumika kama kuzipima nguvu timu hizo baada ya mapumziko ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) hivyo wadau wote wa michezo wameombwa kujitokeza kwa wingi uwanjani ili kuchagia rambirambi ya familia hiyo ambayo kwa pamoja na wanafamilia ya soka walipoteza hazina nyingine muhimu kwenye mpira wa miguu

Post a Comment

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget