Halloween Costume ideas 2015

TANGAZA NASI.

TANGAZA NASI.

KLOPP BADO KICHWA KINAMUUMA NA RATIBA ZA KRISMASI NA MWAKA MPYA.



 

Kocha mkuu wa klabu ya soka ya Liverpool Jurgen Klopp amelalamikia mfululizo wa mechi Ligi kuu nchini Uingereza wakati wa sikukuu za Krismasi hadi kuingia Mwaka Mpya kuwa kunakiporomosha kiwango cha soka nchini England kufanya vizuri katika mashindano makubwa.


Mjerumani huyo amekiri kuwa Wachezaji wa England wana vipaji vikubwa lakini kwa kukosa kwa kukosa kwao mapumziko ya wakati huu wa Majira ya Baridi kutaiathiri England Mwezi Juni kwenye Fainali za Mataifa ya Ulaya, EURO 2016, zitakazochezwa Nchini Ufaransa.

Klopp ameeleza, kuwa England chini ya kocha wake Roy Hodgson, wanapaswa kutwaa EURO 2016 kwa vile wana vipaji vikubwa.

Klopp pia amesema hivi sasa Ligi zote kubwa Ulaya, La Liga ya Spain, Bundesliga ya Germany na Serie A ya Italy, pamoja na nyingine kadhaa,hazina mapumziko ya sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya.

Siku ya kesho Jumamosi Liverpool watakuwa na kibarua kizito watakapokuwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Anfield kuwavaa Vinara wa Ligi Leicester City.

Post a Comment

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

MKRdezign

Contact Form

Name

Email *

Message *

Powered by Blogger.
Javascript DisablePlease Enable Javascript To See All Widget